Hisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 1
()
About this ebook
Read more from Inger Gammelgaard Madsen
Hisia ya Hatia Ichomayo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Tukio la 2: Ruko Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 6 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 5 Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related to Hisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 1
Related ebooks
Hisia ya Hatia Ichomayo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 6 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 5 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPesa Zako Zinanuka Rating: 5 out of 5 stars5/5Mnadhifishaji Tukio la 2: Ruko Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Tukio la 5: Wewe ndiye Unayefuata Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWaliokataliwa: Hadithi Ya Kuchekesha Ya Kisasa Ya Familia Ya Popo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 3 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNajisikia Kuua Tena Rating: 5 out of 5 stars5/5Cheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 4 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJino Kwa Jino Rating: 4 out of 5 stars4/5Robo Mwezi: Watumishi Wa Campoverde Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Tukio la 6: Kunadhifisha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNsungi 2: NSUNGI, #2.1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsDensi Ya Mwezi: Mfululizo Wa Vitabu Vya Kuunganishwa Kwa Damu Kitabu Cha 1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKifungo Cha Bikra Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Tukio la 1: Orodha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPopote Ulipo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKufa na Kupona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Tukio la 3: Jaketi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMnadhifishaji Tukio la 4: Mwongozo Mpya Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPenzi la Damu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTarishi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNsungi 2: NSUNGI, #2.3 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMmeza Fupa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMungu Nisaidie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwanga Wa Usiku: Mfululizo Wa Vitabu Vya Kuunganishwa Kwa Damu Kitabu Cha Pili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMaharagwe Jeli ya Mahusiano Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related categories
Reviews for Hisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 1
0 ratings0 reviews
Book preview
Hisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 1 - Inger Gammelgaard Madsen
purchaser.
Hisia ya Hatia Ichomayo
Sura ya 1
Alipozima gari, gereji yote ilinyamaa. Sauti pekee iliyosikika ilikuwa ya pumzi yake iliyokuwa ya kasi kuliko kawaida.
Taa zilikuwa zimemulika meza ya kufanyia kazi alipoingia. Inaonekana kwamba Lukas alikuwa amefanya kazi kwenye nyumba ya ndege tena bila kuondoa uchafu baada ya kukamilisha shughuli zake. Kulikuwa na mavumbi ya mbao kila mahali na msumeno haukuwa umerejeshwa mahali pake kwenye zana zilizokuwa ukutani. Inaonekana kuwa mwanawe alikuwa amekata tamaa na mradi wake - kwa mara nyingine. Alifurahia kidogo akifahamu kwamba angalau alikuwa amejaribu, na sio kukata tamaa tu na kuketi akitazama televisheni au kompyuta. Wavulana wa umri wa miaka tisa wanapaswa kuwa wepesi kufanya shughuli, lakini yeye hakupenda michezo, sio kama Mia ambaye alifanya mazoezi ya mpira wa mikono mara mbili kwa wiki. Bila shaka, alikuwa mkubwa kwa miaka michache, labda hilo lingebadilika wakati ambapo angekuwa mkubwa kidogo.
Alijipata akiudhika kuwa mwanawe hakuwahi kusikiliza, na kwamba hakuwa amerithi kasi ya vidole ya babake, au tabia yake ya kupenda kuwa na utaratibu. Walikuwa wamechora maumbo ya vifaa vyote kwenye kuta pamoja, hivyo haingekuwa vigumu kupata nafasi ya msumeno. Asidi tumboni mwake ilianza kuchemka na moyo wake ukaanza kupiga kwa kasi zaidi.
Aliegemea nyuma kwenye kiti chake huku mikono yake ikiwa kwenye usukani, kama aliyekuwa bado anaendesha gari, akafunga macho yake, na kujaribu kuzuia kuudhika kwake na hasira. Msumemo haukuwa tatizo. Wala purukushani, au Lukas.
Yeye ndiye aliyekuwa tatizo - kutamauka kwake na maamuzi yake mabaya. Labda kila kitu wakati huo uliopita hakingetendeka, kama angenyenyekea na kumwambia Alice kila kitu. Alihisi kuwa alikuwa amemshuku kwa muda. Alikuwa ameligundua hilo kila wakati alipochelewa kazini, au alipomwambia kuwa alikuwa ahudhurie mkutano ng’ambo. Alikuwa amejua, lakini hakusema chochote. Je, alimpenda kiasi hicho? Je, alifikiri kuwa hakuwa na watu wengine wazuri zaidi waliomtamani kando na yeye tu? Alikuwa mwanamke mrembo, na angempata yeyote aliyemtaka.
Alifungua macho yake na kuyakazia kwenye giza. Wivu ulimchoma ndani mwake alipomfikiria Alice akiwa na mwanaume mwingine. Hilo pekee lilimuonyesha jinsi alikuwa mwanaume aliyestahili dharau. Hakuwa na haki ya kuhisi hivyo, wala ya kuhisi faraja iliyomwingia mwilini alipopita jumba hilo la kifahari na kuona kuwa taa zilikuwa zimezimwa, kumaanisha kuwa Alice na